Sunday 31 August 2014

FAHAMU HATUA TANO ZA HIV MWILINI



Leo tutachambua jinsi Virusi vya Ukimwi (VVU) ambavyo pia hujulikana kama HIV  vinavyoingia mwilini na kujiimarisha. Ni somo gumu lakini tutajitahidi kuelezea ili kila mmoja aelewe. Kuna hatua tano ambazo hufanya Virusi vya Ukimwi kuweza kuingia ndani ya seli za binadamu na kuzaliana.
Virusi hao ambao pia kama nilivyosema hapo juu hujulikana kama HIV hutumia kiasili cha CD4 na wana kama njia ya kupita kwani baada ya mtu kupata maambukizi ya VVU kwa njia yoyote ile navyo kuingia ndani ya mzunguko wa damu wa mwanadamu kuna hatua tano hufuata.
Hatua ya kwanza
Virusi hawa wa HIV huanza maisha yao kwa kuunganisha ncha za protini zilizojitokeza kwenye utando wake zijulikanazo kitaalamu gp120 kwenye vipokeo  vinavyoitwa kitaalamu receptors, vya CD4.
Muunganiko huu wa CD4 na gp120 hubadilisha kabisa umbo la gp120 hali ambayo huruhusu HIV kujipachika katika vipokeo visaidizi  yaani co-receptors vilivyoko kwenye utando wa juu wa seli ya binadamu.
Vipokeo hivi visaidizi hujulikana kitaalamu  chemokine receptors CCR5.
Baada ya hapo, aina nyingine ya ncha za protini zilizo kwenye utando wa nje wa HIV ziitwazo gp41 nazo hubadilika umbo lake, na hivyo kuwezesha HIV kuachia aina nyingine ya protini inayoitwa fusion peptide kwenye seli nyeupe ya damu (white bood cells). Protini hii huwezesha utando wa juu wa HIV kuungana na utando  yaani cell membrane wa seli nyeupe inayoshambuliwa.
Hatua ya pili
 Hatua hii HIV kupenya na kuingia ndani ya seli nyeupe ya binadamu kitendo kinachojulikana kitaalamu  kama Viral Penetration/Fusion. Kitendo cha kuungana kwa utando wa juu wa HIV na ule wa seli nyeupe husababisha kutokea kwa tundu katika utando wa seli nyeupe.
Kitendo hiki huwezesha kibeba vinasaba cha HIV na kusukumwa moja kwa moja mpaka ndani ya seli nyeupe ya binadamu kupitia kwenye tundu hilo. 
Hatua ya tatu
Hao HIV hujivua gamba tendo ambalo hujulikana kama uncoating na husaidia kuruhusu vinasaba vyake  pamoja na vimeng’enyo muhimu kwa ajili ya kubadilisha vinasaba vya RNA kwenda DNA, hatua ambayo husababisha kuzaliana kwa virusi wengine wapya.
Hatua ya nne
 Vinasaba vya RNA hubadilika na kuwa DNA ya virusi kwa kutumia kimeng’enyo cha reverse transcriptase. Kitendo hiki hujulikana kitaalamu kama reverse transcription kwa sababu hutokea kinyume na vile kinavyotakiwa kutokea kwa viumbe hai wengine.
Kwa kawaida, kitendo cha transcription hufanyika kwa kubadilisha DNA kuwa RNA na si kinyume kama chake. Baada ya DNA hii ya virusi kutengenezwa ndani ya ute wa seli ya binadamu, hubadilishwa kuwa aina fulani ya RNA iitwayo messenger RNA, yenye uwezo ya kuamrisha seli kufanya kazi mbalimbali kulingana na mahitaji ya mwili.
Baada ya hapo aina hii ya RNA yenye uzi mmoja hubadilishwa tena kuwa DNA ya virusi yenye nyuzi mbili. Matukio haya yote hufanyika ndani ya ute  unaoitwa kitaalamu cell cytoplasm wa seli nyeupe ya damu.
Hatua ya tano
Hatua hii kitaalamu huitwa integration. Baada ya HIV kufanikiwa kubadilisha RNA yake kuwa DNA, ni lazima sasa HIV aingize DNA hii mpya kwenye DNA ya seli ya damu ili aweze kudhibiti kikamilifu na kuamrisha matendo na kazi zote za seli nyeupe ya damu ili iweze kufanya inavyotaka HIV.

FAHAMU HATUA SITA ZA HIV MWILINI-2






TUNAENDELEA kuchambua hatua sita za tatizo la Ukimwi (HIV) kwenye mwili wa binadamu, endelea.
Ndani kabisa ya kiini au capsid kuna aina tatu tofauti za vimeng’enyo au enzymes ambavyo ni muhimu mno kwa ajili ya uzalianaji wa HIV. Vimeng’enyo hivyo hujulikana kama reverse transcriptase, integrase na protease. Pamoja na vimeng’enyo hivyo, capsid pia ina nyuzi mbili za vinasaba vya RNA ambavyo husaidia kurithisha tabia za vinasaba za HIV kutoka kizazi kimoja kwenda kingine.
Ikilinganishwa na makundi mengine ya viumbe hai yenye vinasaba vingi, HIV ina vinasaba vya aina tisa tu.
Vinasaba vitatu viitwavyo gag, pol na env hufanya kazi ya kubeba taarifa inayohitajika kuunda protein muhimu kwa ajili ya virusi wapya watakaozaliwa.
Vinasaba sita vilivyobaki vinavyojulikana kama tat, rev, nef, vif, vpr na vpu hufanya kazi ya kubeba taarifa ya kuthibiti uzalishaji wa protini inayohusika na kuthibiti uwezo wa HIV kushambulia seli mpya za binadamu, kuzaa virusi wapya au kusababisha magonjwa mbalimbali kwa binadamu.
CD ni kifupi cha maneno ya Kingereza ya cluster of differentiation. Hii ni aina mojawapo ya kiasili kilichoundwa kwa protini na mafuta (yaani glycoprotein) ambacho kinapatikana juu ya uso wa seli nyeupe za damu zijulikanazo kama T helper cells, regulatory T cells, monocytes, macrophages, na dendritic cells ambazo kazi yake kubwa ni kupambana na maradhi mbalimbali. Zimepewa jina la CD4 kuonesha kuwa ni aina ya nne katika kundi la viasili vya CD.
Vilipewa jina hilo mwaka 1984 ingawa viligunduliwa mwishoni mwa miaka ya sabini.
Kazi kubwa za CD4 ni kusaidia baadhi ya chembe nyeupe za damu kupambana na wadudu waenezao maradhi mbambali katika mwili wa binadamu.
Kwa kutumia sehemu yake ambayo ipo ndani ya seli za T cell, CD4 husaidia kukuza na kupitisha taarifa kutoka kwenye vipokeo vilivyopo kwenye T Cell.
Taarifa hii huzitaadharisha chembe nyeupe za damu kujiandaa kupambana na vijidudu vilivyovamia mwili kwa kutumia njia mbalimbali.

1 comments:

  1. I was diagnosed of HSV (Herpes) few years ago and my doctor told me there was no permanent cure for the disease. I was given medication to slow down the progress of the virus. At the initial stage it was not so bad till it progressed to a stage were i had difficulties going about my daily activities because i constantly felt pains in my penis, and around my genital were i had these blisters. I was totally devastated and i was even ashamed to complain to anyone. I saw a publication about a doctor called Dr.Water, and from what i read, he was using herbal medicines to cure illnesses like HERPES, Human papillomavirus, ALS, Diabetes, HIV, and so on. I opted to contacted him via email, after a few dicussion, i ordered for his medicine. He prepared the medicine and shipped it to me. When i received the herbal medicine, I took it according to his instructions. After using it as instructed, few weeks later i went to the hospital to have a blood test and the test came out negetive. To my greatest surprise, i was cured of this stubborn virus just by using a simple herbal product.
    That is why i am here sharing my testimony as much as i can to create as much awareness as possible so that people can also benefit and be cured too. contact him for help, via his email: {DRWATERHIVCURECENTRE@GMAIL.COM} or WhatsApp (+2349050205019). this is my persona email: marianosuarezsm@gmail.com, you add me on hangout

    ReplyDelete